SOMO: KUTAHARAKISHA KWA KUSUDI LA MUNGU
MHUBIRI: Pst, Dr. Eva Mbise | 09/02/1015
UTANGULIZI:
KUTAHARAKISHWA
(QUICKEN), Ni kutokutulia/ kutokuwa na amani. Kunakuwa na nguvu inayokuwa ndani
isiyokuacha utulie; kutokea ndani yako na kukulazimisha kufanya mambo.
Nataka
kuzungumza kwa Habari ya Nguvu inayokaa ndani yetu inayotakiwa kufanya kazi kwa
ajili ya Mungu kwa kile kitu alichoweka ndani ya kila mmoja.
Kila mtu
anafahamu kuna kitu kimewekwa ndani cha Ki-Mungu atakama tulizaliwa kwa Bahati
mbaya (wengine wanaseema mtoto wa Nyongeza) kwa Mungu hakuna Bahati Mbaya.
Ni kazi ya
Roho Mtakatifu tunayempokea kupitia Kristo Yesu kukaa ndani yetu lakini hawezi
kunyamaza huku ndani yetu, anataka kitu cha Ki-Mungu kifanyike ndani yetu. Hivyo
ni kazi yake kukisukuma hicho kitu kitoke ndani yetu kuja nje ili
kutudhihirishia ulichokibeba.
ukikaa na
kutulia tu hatuwezi kuona kile ulichobeba. Hivyo Roho Mtakatifu anapokaa ndani
yako na kusukuma kile kitu ndani yako ndipo tunaona lile kusudi lililowekwa
kwako.
Kipi kinachokutaharakisha?
1. Ni moja ya kazi ya Roho Mtakatifu
anapokuwa ndani yako kukutaharakisha; kukupeleka katika majukumu ambayo MUNGU
amekusudia kuweka ndani yako
2. Ni kazi ya Roho Mtakatifu kutusukuma,
kutunyima amani, kutukosesha utulivu mioyoni mwetu ili kutizima azima nzima ya kuumbwa kwetu.
3. Roho Mtakatifu anakuwa kichocheo cha
kutokutulia ndani yako huku akisukuma kwa mzigo kile ulichoumbiwa kukifanya
kutokea nje.
Matendo ya Mitume 9:15 – 16 SUV
15. Lakini
Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue
Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.
16. Maana
nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.
Huu ni uchaguzi wa mtumishi wa Mungu Paulo zamani akiitwa Sauli. Kipindi
akiwa Sauli alitumikia kusudi lakini katika mlango m’mbaya. Kristo akakutana
nae na akamgeuza ili atumikie Kusudi lakini katika mlango mzuri.
Anayeambiwa hivi anamjua Paulo, anamjua anafanya nini hvyo anamwambia
Mungu huyu hafai katika kazi hii. Lakini MUNGU anamwambia mtu huyu nimemchagua
mimi. Nenda muonyeshe yampasayo kufanya.
Tazama ‘15. Lakini
Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue
Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.”
Haleluya!!!
Kwa wakati ule Kristo hakuona mtu
mwingine mwenye kusudi aliyeumbwa achukue Jina la Mungu na kupeleka kwa mataifa
hofu ilikuwa kwa kanisa. Lakini Paulo kwa sababu aliumbwa kwa wakati ule; hiki
ni chombo changu nenda kanitakasie, utakapomtakasa/ mtenge usiache kumwambia
yatakayomkuta. Tazama “16. Maana nitamwonyesha yalivyo mengi
yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.”
Kwa wito ulioitiwa hakuna tu Raha, hakuna tu Pumziko hata kama kanisa la NENO
LA NEEMA wamesema NI MWAKA WA KUTANUKA; inawezekana wenzako wakawa wanatanuka
lakini wewe unatanuka katika mateso.
Kumbuka Paulo alikuwa mahali anaomba, akaja nabii wa Bwana aitwa Agabo
akachukua mkanda wa mtu aitwae Paulo akafunga kiunoni mwake akisema, “ Hivi
ninavyo funga huu mkanda, mwenye huu mkanda vipigo vinamsubiri…” Matendo 21:11
Paulo akasema najua KUSUDI nililoitiwa hivyo sitishwi na vipigo
vilivyombele maana tangia kuitwa niliambiwa vitisho vilivyombele… nakuambia mtu
mmoja anayefikiria kwa Mungu ni mteremko; kwa Mungu ni shwari… Shwari ipo
lakini WITO wako unavitu vyake; pale unapopita kwenye mapito MUNGU anataka
kujivunia wewe, unapopita anataka kusikia wewe ukisema NIMEMUONA, ANAPONYA,
ANAINUA…
Ona Agabo anamwambia Paulo unaenda kuonana na haya kesho, lkn Paulo
anasema siogopi kuhusiana na hayo hata kama nikufa nipo tayari.
Kutaharakishwa na kusudi kwanza, ukubali maumivu, ukubali kupoteza Jina
lako, Ukubali watu wakutenge, wakukatae. Hata kama watu/ dunia yote ikatae
kukaa na wewe lakini uko tayari kusimama na Mungu bado utasimama.
Naongea na Mtu eh! Haleluya…
Kila kusudi lina wito wake ndani. Hatuwezi kupanda UZURI
kwenye UBAYA, lazima tung’oe ubaya ili tupande Uzuri.
Yeremiah aliitwa kwenye kusudi (Yeremia 1:10).
Kumbuka Paulo aliitwa abebe jina la Kristo kwa Mataifa, Yeremia aliitwa kuwa
nabii wa Mataifa na Wafalme. Kutokana wito wake aliishia gerezani.
Lakini hawakuzuia kusudi lake huko
walipomuweka maana kusudi halizuiliki.
Kila mtu amebeba kusudi ndani yake na kama hujui inabidi ukae chini
ujiulize kwa karibu.
Wagalatia
1:15 -16
Lakini
Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake,
Paulo aipogundua kusudi alijiambia mwenyewe ndani yake Mimi nimeitwa kwa
ajili ya hili kusudi lazima niwaambie watu Habari ya Injili ilivyobadilisha
maisha yangu. Lengo nikaitoe kwa watu.
Roho Mtakatifu nimekwambia kazi yake ni kusukuma hilo kusudi wewe
ukijifanya umenyamaza utashangaa unaanza kuota ukihubiri Habari njema za Bwana YESU
KRISTO, ukiangalia kioo unaona mataifa ukiyahubiria ‘Njooni kwa Yesu!’ ujue
tayari ni msukumo wa Kusudi.
-
Ukiona
mtoto anaanza kuomba na Kubandikia
wenzake mikono tambua kwamba kuna kitu klipo ndani unatakiwa kukilea.
-
Ukiona
mtoto ameamka na anafuata BIBLIA na kuanza kusoma hata kama hajui kusoma
mwachie anapoangalia kuna mambo huishwa ndani yake.
Haleluya!! Nina mtu anakusudi hapa?
Waamuzi
13:24 – 25
24. Basi
yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni, mtoto huyu
akakua, BWANA akambarikia.
25. Roho
ya BWANA ikaanza kumtaharakisha katika Mahane-dani, katikati ya Sora na
Eshtaoli.
“Mbingu inapotafuta kufanya jambo hapa duniani inaangalia
tumbo la mtu alietayari na kuweka uzao wenye kusudi hata kwa jambo la miaka
25 mbele”
Kusudi la kuzaliwa kwa Samson lilikuwa Bwana ajilipizie
kisasi. Hivyo yeye hakuwa na kuogopa lolote. Kumbuka kusudi haliombwi, kusudi hatulifungii!.Kusudi
tunazaliwa nalo, Kusudi linatokea ndani
yetu.
Samson,
akavaliwa na kusudi la kulipiza kisasi; akiona watu kunaibuka hasira. Akiona
watu wanatesa kanisa la Bwana inalipuka kulipiza kisasi. Sio yeye ni kusudi.
Ukimwangalia mtoto wako unaona nini?
Ukijiangalia
unaona nini? Kwa sababu kinachokutaharakisha ni kile unachoona ndani.
Ukiona upo nyoronyoro sana TAFUTA KUSUDI.
Isaya
58:1 – 14
1. Piga
kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; Uwahubiri watu wangu kosa lao,
Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.
Isaya
61:1- 3
1. Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa
sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma
ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao
waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.
2.
Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha
Mungu wetu; kuwafariji wote waliao;
è Hakuna
Utukufu katika vitu BALI kuna utukufu katika KUSUDI. Unapolitumikia kusudi,
kusudi huachialia Utukufu. Kadri unavyoishi/ Kudumu katika kusudi ndivyo Mungu
anavyoachilia UKUU, HESHIMA, UTUKUFU, NAFASI N.K
è Kuna
watu leo hawaoni furaha ya WOKOVU, hawaoni maongezeko na kutanuka; yaani
wamedumaa na wamekuwa sababu ya kulaumu oh MUNGU hajibu, Mungu hasemi… Upo
katika kusudi lipi ambalo leo akija anakukuta mko na Usemi.
Mf. Umeajiriwa mahali (Mkuu wa ofisi na Mwajiriwa) wao huwasiliana mara
kwa mara kwa kuonana na kupigiana simu kwa sababu ya uunganiko wa kazi, Vivyo
hvyo nasi jatika Ufalme. Mungu huongea sana tu na Marafiki zake.
Matendo 20:22 – 24
22. Basi sasa, angalieni, nashika
njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta
huko;
23. isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba
vifungo na dhiki vyaningoja.
- Nakumbuka tulipokuja mara ya kwanza Kibaga, Kinyerezi
(Mahala tulipoweka HEMA la KUKUTANIKIA) mimi na Hefsiba hapakuwa na mazingira
mazuri palikuwa kumejaa maji lakini tulipozunguka eneo, tukaambiana hivi
“Panatufaa” japokuwa panaonekana pako duni, pamekufa lakini sisi tumejaa uhai
tupachukue.
Wenzetu tunawaambiaje hapa, nkamjibu tusiogope na
tulipowaambia tuliitikiwa vizuri na kupata hela ya kupachukua na leo unapaona
vile kulivyoo sasa nab ado hakujafikia vile viwango tulivyovioona.
Nataka nikutangazie Leo, kwa ajili ya kusudi piga hatua
nenda mbele na ujisemeshe kuwa ninaweza, mimi ninamiliki hapa!
Mwenye kusudi HUPISHWA; watu hunyanyuka kwenye viti na
kupisha wenye kusudi.
Usiniambie nimezaliwa katika familia duni au nimezaliwa
familia isiyofaa; kwa sabubu hiyo siwezi kuwa kile natakiwa kuwa, nitakujibu akili
yako ndio imekufa wala akili ya Kristo haipo ndani yako lakini Mungu huinua akili zilizokufa na kuzipa kufanya
kazi upya.
“… Katika
kusudi hakuna jambo jepesi”
Yoeli 2:28 -29
28. Hata itakuwa, baada ya hayo, ya
kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa
wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;
29. tena
juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho
yangu.
Matendo ya Mitume 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha
kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika
Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
2 Timotheo 1:7
7. Maana Mungu
hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
8. Basi usiuonee haya
ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie
mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu;
- > Wewe una Roho wa Bwana ndani yako, ambaye ana uwezo,
Nguvu anainua mambo mapya, haombwi huyu yupo ndani yako.
Kipi kinachokuogopesha?; Kipi kinachokuumiza?. Unae ROHO wa
BWANA
è
Kwa nini tuishi kwenye KUSUDI sasa?
Kuambukiza Tamaduni za Ufalme wa Mungu
katika mazingira tunayoishi. Kama vile koloni zilivyotuambukiza taratibu zao
vivyo hivyo na tamaduni za ki-Mungu lazima tuziambukize.
(i)
Kuwa na Tabia/Maamuzi na mikao ya KiMungu ktk
maisha yetu
(ii)
Kutengeneza watu wenye Tabia za Ufalme wa Mungu
mahali tulipo.
(iii)
Kuathiri mikao ya Wana wa Mungu kwa tamaduni za
Kifalme
Kuna watu tunaenda Hospitali
kutembelea watu/ jamaa / ndugu na marafiki lakini hatuwaambi watu hapo Habari
njema.
Kuna watu tunapanda daladala kila
siku lakini hatusemi habari za Ufalme wa Mungu
Jiulize
na Tafakari kwa kina juu ya KUSUDI LAKO.
Kusikiliza na kutaza fundisho hili kwa youtube
Umebarikiwa!!!
Kwa mafundisho haya na mengine mengi usisite kutufuatilia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii bofya hapa
Comments
Post a Comment